UONGOZI SIMBA SC WAOMBA RADHI KWA MARA NYINGINE TENA

MENEJA wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, amewaambia mashabiki wa timu hiyo kuwa, wanatakiwa kusahau matokeo ya Kariakoo Dabi na badala yake wajipange kwa ajili ya michezo ya Ligi Kuu Bara, kwani bado wana kikosi imara.

Bosi huyo ameyasema hayo ikiwa ni siku chache baada ya kutoka kufungwa 2-1 dhidi ya Yanga katika mchezo wa Ngao ya Jamii uliochezwa wikiendi iliyopita kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar.

Akizungumza na Spoti Xtra, Ally alisema: “Wanasimba tumepoteza Kariakoo Dabi, hayakuwa malengo yetu msimu huu, hivyo tutulie na tuungane kwa pamoja tukianza msimu mpya ambao ninaamini unakwenda kuwa mzuri kwetu.

“Kama uongozi tunaamini haitakuwa rahisi kusahau, lakini tunapaswa kujisahaulisha maana ligi ndio inaanza, kikubwa tuwaachie kazi benchi la ufundi kwani wao ndio wanatengeneza timu ya ushindi, uzuri ni kwamba tayari wameona upungufu uliopo, hivyo watafanyia kazi yote.”

Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0753 336 000

Masengwa blog Ipo Play Store…Download HAPA ,Uwe unapata habari zote kwa urahisi zaidi
 Bofya Hapa

No comments:

Powered by Blogger.